Quantcast
Channel: JamiiForums | The Home of Great Thinkers
Viewing all articles
Browse latest Browse all 12945

Madhaifu 8 uliyonayo na watu hawawezi kukwambia

$
0
0
Habari wana JF! leo ni mara yangu ya kwanza kuandika thread humu toka ni join 2011, Nimekuwa msomaji mzuri sana wa thread mbalimbali, haswa zile zinazohusu maendeleo. mimi sio mwandishi wala sio mtu mwenye ujuzi yakinifu katika maisha.Nitazungumzia mambo 8 sisi sote hufanya makusudi au kwa kutokujua. Mwaka 1955, bw. joseph luft na harrington waligunda tafiti inayoitwa "Johari Window" hi ime base jinsi binadamu tunavyowasiliana na utambuzi binafsi wa mtu. Johari window imegawanyika katika tabia 4 kuu.
  1. Tabia inayojulikana kwetu na kwa wengine.
  2. Tabia inayojulikana kwetu na sio kwa wengine.
  3. Tabia isiyo julikana kwetu na kwa wengine.
  4. Tabia inayojulikana kwa wengine na sio kwetu.

leo ntaongelea tabia ya 4. Tabia iambazo watu wanazijua ila sisi binafsi hatuzitambui kabisa. Nilipo gundua uwepo wa "Johari window" ilinisumbua sana kwa kujiuliza yawezekana vip mimi nisijitambue tabia zangu, ila wanao nizunguka wanazifahamu? na haswa zile tabia mbaya(hasi). Kwenye thread/makala nitataja mambo 8 hasi(negative) niliyo yagundua toka kwa watu mbalimbali kama:wafanya kazi,marafiki,ndugu hata kwenye mkusunyiko wa watu msio juana, mkawa mnajadili jambo flani au hata humu pia jamii forum. Tunabidi tuzitambua hizi tabia hasi kwenye maisha yetu kama tunataka mabadiliko ya kweli.
  1. Wewe ni hasi(negative)

Je, umewahi kugundua kwamba kama mtu anakwambia kitu, iwe juu yao wenyewe au mtu mwingine, wewe hujibu kwa maoni sarcastic au kusema kitu hasi? Aina hii mbaya ya reaction inaweza kuwa kutokana na ukweli kuwa wewe ni pessimist, na inaweza kuwa kwa sababu ya wingi wa sababu, ikiwa ni pamoja na kukosekana kwa usalama wivu, wivu,n.k ukijikuta wewe ni pessimist, (hufikiria siku zote glasi haina maji) jaribu kuacha na fikiria kwa nini unakuwa na mawazo hasi. Ukiweza kuelewa sababu za negativity yako, unaweza kuwa na uwezo wa kupambana nayo kabla hujakimbiza marafiki na familia mbali, kwa sababu hakuna mtu anataka kuwa karibu na mtu pessimist wakati wote. 2. Wewe si msikivu Je, hukatiza watu wakati wa mazungumzo? Kama ni hivyo, unaweza kuwa na sio msikilizaji mzuri. Kusikiliza ni muhimu kama kuzungumza linapokuja kudumisha mahusiano ya afya. Kuwa rafiki mzuri kwa mtu, ni muhimu kusikiliza kile anacho kisema, bila kujali ni kiasi gani unaweza kutokubaliana nao. Kama husikilizi, watu hawato kuja kuzungumza na wewe, na hatimaye wewe kuwafukuza. Kusikiliza ni njia kwa wewe kuelewa jinsi rafiki au familia inaweza kuwa na hisia, na kusikiliza unaweza kwenda njia ndefu ili kuwasaidia kujisikia vizuri au zaidi kwa urahisi. 3. Unaongelea sana kuhusu maisha yako Je, umewahi kugundua kuwa hupiga simu au kuwatumia msg watu wakati unataka kuwaambia habari kuhusu kitu kilichotokea au kuwaambia habari kuhusu wewe mwenyewe? Kama ni hivyo, unaweza kuwa ni mtu ambaye anazungumza mambo kuhusu wewe mwenyewe sana, na narcissist haina furaha kwa wote. Unapo jizungumzia mwenyewe sana, watu huboreka na kujaribu kukaa mbali na wewe. Ili Kudumisha uhusiano wa afya na rafiki au familia, unahitaji kuzungumza na vilevile kusikiliza kiasi sawa. Unaweza ongelea habari kuhusu wewe mwenyewe, lakini hakikisha kuwa una msikiliza mtu mwingine ili wote kupata kiasi sawa ya muda majadiliano. 4. Attitude yako ni mbaya Kama watu wanamatatizo na tabia zako au jambo lolote na hawaoni sababu ya kukwambia kuwa una wa kwaza, ni kwasaba unaweza kukasirika kwa sabau una attitude problem. ukionyesha watu attitude yako,inaweza kuwakera na hata kuwa ngumu kushirikiana na wewe. Hamna mtu anaetaka kukaa na mtu mwenye attitude mbaya. jaribu kuwa mtu anaefikika, na kama umemkera mtu na akakwambia usikasirike chukulia ni njia ya kujirekebisha. 5. Maisha yako ni Tamthilia Wakati mwengine unadhani maisha yako ni kama isidingo..!Naam pengine sio hata kidogo. Na ukweli ni kwamba wakati unaamini ni tamthilia taratibu unawafukuza watu kwenye maisha yako. jambo likitokea kwako, haipaswi kuwa au kulifanya jambo kubwa. unless ukifanye kiwe kikubwa. ulishasikia msemo unaosema making a mountain out of a mole hill?Kama wewe ni mtu ambaye huchukua maisha yako kwa umakini mno au hufanya kila kitu kuwa kikubwa, Basi unatengeneza mlima kwenye mole hill. Kushughulika na hali ya maisha kwa utulivu na kwa nidham daima kuwa na manufaa zaidi kuliko kujenga hoja juu ya mambo kuwa na msingi kwa wenzako. 6. Umekombatia shida(fikra duni) kama wewe ni mtu mwenye fikra duni au unawaza shida, unaweza ambukiza shida zako kwa rafiki zako ,ambao wataanza kuwa hesitant kuwa karibu yako. wewe unakuwa ni mtu wa kubisha bisha tu, bila sababu za msingi. hamna mtu anaetaka kukaa na mtu mwenye negativity na fikra duni. tafuta kitu cha kukupa furaha, ili kusahau hida na hakikisha hautangazi kwa mtu. 7.Maneno unayozungumza(umbea) watu watakupotezea kama (babu loliondo) wakijua kuwa wewe ni mmbea, yes umbea unaraha yake na uchekesha karibu kila mtu anafanya kwa wakati wake. ukiwa mbea watu wataacha kukwambia mambo yao. kama unajua jambo kuhusu mtu, mfwate mwambie au kaa kimya. 8. Huna huba ya kukabiliana na hisia za watu Unaweza kuwa mkweli, kwa ni jambo jema, inaweza kuwa ni lenye kuumiza na inaweza kusababisha kupoteza marafiki. Wakati kutafuta na kudumisha uhusiano wa afya unahitaji kuwa na ufahamu wa hisia za watu wengine. Baadhi ya watu inaweza kuwa na hisia zaid wakati wengine wanaweza kuwa hawana , lakini hata hivyo hakikisha unatumia busara. Tact inaweza kuokoa kutoka kuonekana kama mtu mbaya na inaweza kuhakikisha kuto umiza hisia ya mtu. Ni rahisi sana kujua mapungufu ya mtu, kuliko kuyajua yetu. lakini kama tunaweza kuyajua ya wenzetu basi pia sisi tunayo. na pale tunapo baini mapungufu inatupaswa kuwa na positivity na kurekebisha yale tutakayo weza. Naomba Radhi kwa maneno ya kiingereza. I will be posting more about personal development. Sote tuelimike na tubadilishe maisha yetu.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 12945

Trending Articles