Quantcast
Channel: JamiiForums | The Home of Great Thinkers
Viewing all articles
Browse latest Browse all 12945

Al-Shaabab wafanikiwa kulipua jengo la makazi ya Waturuki...

$
0
0
Gari lililokuwa limesheheni milipuko lililipuka katika
milango ya makazi ya Waturuki katika mkoa wa
Hodan, lililoua mlinzi Mturuki na Msomali aliyekuwa
karibu na hapo, na kuwajeruhi wengine wengi. Wanamgambo watatu wa al-Shabaab, ikiwa ni
pamoja na mlipuaji wa gari, pia waliuawa na kutangulia mbele ya haki. Serikali ya Uturuki imelaani shambulio hilo "katika
matamshi makali kabisa inayowezekana" na Waziri
wa Mambo ya Nje Ahmet Davutoglu alituma salamu
za rambirambi kwa familia za waliofariki katika
akaunti yake ya Twitter. "Ninasikitika kwa shambulizi lililotokea huko
Mogadishu karibu na Ubalozi wa Uturuki -
tunapambana kuondoa hali hii ya vurugu kutoka
Somalia," Waziri Mkuu wa Somalia Abdi Farah
Shirdon alisema katika Twitter Jumamosi. "Imetushtua kusikia shambulio la ugaidi kwa
Waturuki wenzetu," Nicholas Kay, mkuu wa Misheni
ya Misaada ya UN nchini Somalia (UNSOM), alisema
katika Twitter Jumamosi. "Nawapa pole sana.
Vurugu hazitafanikiwa. UN inaungana na Uturuki
na Somalia." Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Marekani
Jen Psaki alilaani mashambulizi na kupongeza
majukumu ya Uturuki nchini. "Kitendo hiki cha kinyama hakitashirikisha wajibu
wetu wa kuendelea kufanya kazi kwa ajili ya
amani, demokrasia zaidi na mafanikio ya siku zijazo
ambazo wasomali wanastahili," alisema. Al-Shabaab kwa haraka na kujivunia tukio hilo ilichukua dhamana kwa
shambulio katika mfululizo wa matamko
wanayoyatoa katika Twitter. "Uturuki ni sehemu ya kundi la nchi zinazosaidia
mfumo usio na dini na wanajaribu kukomesha
uanzishaji wa Sharia ya Kiislamu," al-Shabaab
ilisema katika Twitter. Uturuki imefadhili miradi mingi ya maendeleo nchini Somalia kwa miaka michache iliyopita, na kuandaa mazungumzo ya umoja kati ya Somalia na mkoa wa Somaliland mwezi huu. Al-Shabaab imekuwa ikiongeza mashambulizi yake wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhan, ikijigamba kuhusu mauaji ya idadi kadhaa ya watu...

Viewing all articles
Browse latest Browse all 12945

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>